Proverbs 2:1-9

Faida Za Hekima

1 aMwanangu, kama utayakubali maneno yangu
na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
2 bkutega sikio lako kwenye hekima
na kuweka moyo wako katika ufahamu,
3 cna kama ukiita busara
na kuita kwa sauti ufahamu,
4 dna kama utaitafuta kama fedha
na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
5 endipo utakapoelewa kumcha Bwana
na kupata maarifa ya Mungu.
6 fKwa maana Bwana hutoa hekima,
na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
7 gAnahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu,
yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
8 hkwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki
na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.

9 iNdipo utafahamu lipi lililo kweli na haki
na sawa: yaani kila njia nzuri.
Copyright information for SwhNEN